February 25, 2015


Ile ishu ya kiongozi mmoja wa Simba kuzuiwa kuingia kambini, imezidi kuchukua sura mpya.  Hii ni baada ya Makamu Mwa Simba, Geofrey Nyange ‘Kaburu’ kufunguka baada ya kuwa na taarifa kuwa yeye ndiye mlengwa.


Hivi karibuni vyombo mbalimbali vya habari vimekuwa vikiripoti kuwa kuna kiongozi amekatazwa kuitembelea kambi ya timu hiyo kutokana na kuhusishwa kumpangia kocha timu.

Baadhi ya vyombo vya habari vilimtaja kiongozi huyo ambaye amefungukia ishu hiyo.

Kaburu ambaye pia ni Mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), amesema kwamba taarifa hizo hazimhusu yeye kwa kuwa yeye kwanza hana tabia ya kwenda kambini na pia hilo si jukumu lake, hivyo si kweli kwamba yeye ndiyo mlengwa wa kuzuiwa huko.

Alifafanua kuwa yeye ana majukumu yake ndani ya timu hiyo na si ya kuitembelea timu inapokuwa kambini kwa kuwa watendaji wa masuala hayo wanajulikana na pia kama ingekuwa amesimamishwa kwa mujibu wa taratibu zilivyo, ni lazima angeitwa na kuambiwa hata katika kikao chao cha viongozi.

“Sijazuiwa na wala sijaambiwa chochote kuhusu mambo ya kwenda au kutokwenda kambini kwa sababu kwanza mimi si mtu wa kwenda kambini mara kwa mara kwa ajili ya kuitembelea timu, isipokuwa huwa nakwenda huko kama inatokea kuna kikao cha viongozi na timu nzima.

“Kama ingekuwa ni kweli nimezuiwa kufika baadhi ya sehemu na uongozi basi ningeambiwa tu lakini mpaka sasa sina taarifa yoyote, kwa hiyo ina maana si mimi mlengwa wa suala hilo, mimi kazi yangu ni majukumu ya kiofisi tu na si mengine kama hayo ninayoambiwa kuwa nimekatazwa kufika kambini.

“Pia hizi taarifa za kumpangia kocha kikosi si za kweli, mimi siwezi kufanya hivyo kwa kuwa hiyo si kazi yangu, ni kazi ya kocha, kocha ameletwa kwa ajili ya kazi hiyo kwa hiyo siwezi kumuingilia kwenye majukumu yake.

"Ila naweza kupiga stori na kocha kuhusu wachezaji aliowachezesha na kumuuliza kwa nini alimchezesha huyu na kumuacha yule, basi, na si vingine, na hiyo kuzungumza na mwalimu kuhusu masuala hayo si kumpangia kikosi ila ni kama unahitaji kujua tu,” alisema Kaburu.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic