Mtibwa Sugar imezidi kuonja
joto ya jiwe katika jiji la Dar es Salaam, safari hii ikikumbana na kipigo cha
aibu cha mabao 5-2 kutoka kwa Azam FC.
Katika mechi hiyo kwenye
Uwanja wa Azam Complex, Chamazi jijini Dar, Mtibwa ilipata kipigo hicho cha
pili mfululizo baada ya kuwa imelala kwa mabao 2-0 dhidi ya Yanga katika mechi
iliyopita.
Wachezaji wawili wa zamani
wa Yanga, Didier Kavumbagu na Frank Domayo ndiyo waliokuwa mashujaa baada ya
kila mmoja kufunga mabao mawili.
Bao la tano lilifungwa na
raia wa Ivory Coast, Kipre Tchetche.
Hadi mapumziko Mtibwa Sugar
ilikuwa nyumba ka mabao 3-1, mawili yakifungwa na Kavumbagu, moja Domayo na wao
Mtibwa wakiwa wamepata bao kupitia Salum Mpakala.
Kipindi cha kwanza ndiyo
kilikuwa kigumu zaidi kwa Mtibwa waliomaliza mzunguko wa kwanza wakiwa
wanaongoza ligi kuu.
0 COMMENTS:
Post a Comment