February 11, 2015



Wapinzani wa Mtibwa Sugar katika mechi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, El Merreikh ya Sudan inatua kesho na moja kwa moja kwenda kufikia katika moja ya hoteli kubwa nchini ya nyota tano ya Serena.


Merreikh inatarajia kutua nchini saa 7 mchana tayati kwa mechi yao ya kwanza dhidi ya Azam FC kwenye Uwanja wa Azam Complex, Chamazi jijini Dar.

Timu ni moja ya zile tajiri zaidi barani Afrika na ina uzoefu mkubwa wa michuano iliyo chini ya Shirikisho la Soka Afrika (Caf).


Hata hivyo, Azam FC wameonyesha wako sawa na wanawasubiri kwa hamu baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 5-2 dhidi ya Mtibwa Sugar.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic