Mbunge wa Mbeya mjini
kupitia Chadema, Joseph Mbilinyi maarufu kama Sugu, leo alimkaribisha
mwenyekiti wa chama hicho kwenye Uwanja wa Sokoine mjini Mbeya.
Sugu alimkaribisha kushuhudia timu anayoishabikia kutoka jimbo lake ya Mbeya City wakati ikicheza mechi ya kirafiki dhidi ya Yanga.
Ilikuwa mechi ya Ligi Kuu
Bara na Mbowe alikuwa kati ya mashabiki walioshuhudia Mbeya City ikitandikwa
mabao 3-1 licha ya kuwa nyumbani.
Sugu aliungana na mashabiki
jukwaani kama ilivyo kawaida yake lakini haikumzuia kuona mabao matatu ya Simon
Msuva, Mrisho Ngassa na Mrundi Amissi Tambwe yakiididimiza timu yake nyumbani,
tena mbele ya mgeni wake.
0 COMMENTS:
Post a Comment