Ken Oliech ameamua kugombea
nafasi ya Mwenyekiti wa Shirikisho la Soka Kenya (FKF).
Sam ni kaka wa mshambuliaji
wa Ajaccio ya Ufaransa, Denis Oliech.
Kwa sasa nafasi hiyo
inashikiliwa na mkongwe Sam Nyamweya ambaye amekuwa katika malumbano makubwa na
wenzake.
Sam ambaye aliwahi kuwa
mmoja wa mabeki gumzo nchini Kenya, amesema anaamini atachangia maendeleo ya
soka kwa kusaidia mabadiliko.
“Soka la Kenya sasa
linahitaji mabadiliko, linahitaji vijana, sura mpya na mawazo mapya.
“Miaka mingi sasa watu
wamekuwa ni walewale na hakuna mabadiliko. Sasa ni wakati mzuri kufanya
mabadiliko kwa lengo la kusaidia mpira wa Kenya,” alisema Sam.
0 COMMENTS:
Post a Comment