February 2, 2015


Kocha Msaidizi wa Simba, Selemani Matola amebadili uamuzi wake wa kutaka kuondoka klabuni hapo baada ya bosi wake, Goran Kopunovic kusisitiza: “Haondoki mtu.”


Habari za uhakika kutoka Simba zimeeleza, Kopunovic aliutaka uongozi wa Simba kumuacha azungumze na Matola ambaye aliueleza uongozi wa klabu hiyo ameamua kuondoka katika timu kubwa.
“Kweli, kocha alisema asingependa kumuacha Matola ambaye amekuwa mchapakazi na mtu anayejua kuifanya kazi yake.

“Hivyo aliuomba uongozi azungumze na Matola halafu atawapa jibu, kweli alifanya hivyo na mwisho wakaelewana.

“Hata baadhi ya viongozi nao walimfuata Matola na kuzungumza naye kuhusiana na suala hilo na kumsihi abadili uamuzi,” kilieleza chanzo cha uhakika.

 “Nataka nikuhakikishia, Matola hana tatizo, hata wale mashabiki waliomzomea hawajui lolote. Viongozi wanaotaka maslahi ya Simba wanajua umuhimu wake na anavyojituma.”

Alipotafutwa mwenyewe Matola, alipokea simu na kusema: “Kwa sasa naomba mniache kidogo, nitalizungumzia vizuri siku nyingine.”

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic