Straika Charlie
Austin wa Queens Park Rangers amemtolea uvivu kiungo mkongwe wa timu hiyo Joey
Barton kwamba aliwaponza.
Barton
alitolewa kwa kadi nyekundu katika mechi dhidi ya Hull City baada ya kumpiga
kwenye korodani kiungo Tom Huddlestone.
Barton alifanya
kitendo hicho ikiwa ni baada ya kumchezea madhambi beki Alex Bruce.
QPR ilipoteza
mechi hiyo baada ya kuwa imetangulia kwa bao la Austin ambaye baada ya kufunga
aliigiza kama mlemavu.
Barton
anaaminika mmoja wa wachezaji wakorofi zaidi katika Ligi Kuu England.
0 COMMENTS:
Post a Comment