Na
Saleh Ally
BAADA
ya soka, mchezo wa ngumi ndiyo wenye mashabiki wengi zaidi nchini. Inawezekana
hii ikawa kwingine kote duniani ingawa nchi nyingine zina aina nyingi ya
michezo iliyo hai.
Hakuna
ubishi kuthibitishwa kwa pambano la wakali wawili wa mchezo wa ngumi duniani
Floyd Maywether dhidi ya Manny Pacquiao ni mtikisiko wa maswali mengi
yasiyokuwa na majibu hadi hapo itakapowadia Mei 2, mwaka huu kwenye Ukumbi wa
MGM Grand jijini Los Angeles, Marekani.
Wawili
hao wamekubali kupanda ulingoni katika pambano hilo linalochukua historia ya
kuwa pambano la kufunga midomo na ghali zaidi katika mchezo wa ngumi kwa kuwa
litagharimu zaidi ya dola milioni 250 (Sh bilioni 425).
Kati
ya fedha hizo, Mayweather atachukua dola milioni 150 (zaidi ya Sh bilioni 255)
huku Pacquiao kutoka Ufilipino akiondoka na dola milioni 100 (zaidi ya Sh
bilioni 170).
Pambano
hilo limekuwa katika mjadala kwa miaka mitano sasa, huku kila mmoja akionyesha
kuwa na hofu na mwenzake.
Wakati
fulani, ilifikia Pacquiao ambaye ni mbunge kukubali kucheza lakini akagoma
kutekeleza pendekezo la Maywether kumtaka apimwe kama hutumia dawa za kuongeza
nguvu au la.
Kukataa
kwa Pacquiao, kulifanya pambano hilo liendelee kuwa hadithi kwa muda huo lakini
sasa kinachosubiriwa ni ndondi na si vinginevyo kwa kuwa Pacquiao amekubali
kupimwa, kitu ambacho awali aliona ni kama kudhalilishwa.
Kila
mmoja amekuwa akitamba kivyake lakini ukweli au jibu sahihi ni Mei 2 kwenye
Ukumbi wa MGM Grand Garden Arena. Pambano hilo ni ghali zaidi kutokea katika
mchezo wa ngumi na mara tu baada ya mabondia hao kusaini mkataba huo, fedha
zimeanza kumiminika.
Makampuni
mawili maarufu ya runinga, maarufu katika kuonyesha mchezo wa ngumi ya HBO na
Showtime, yamekubali kutoa mamilioni ya fedha kuonyesha pambano hilo.
Nini kinachovuta?
Wengi
wanajiuliza ni kipi hasa kinachowachanganya wengi? Mabondia hao ndiyo bora
zaidi katika kizazi cha sasa ulingoni.
Hakuna
aliyetarajia siku moja wangekutana katika ulingo mmoja. Baada ya chenga za
miaka mitano, sasa wanakutana na ubishi utamalizwa.
Rekodi
zao pia ni chanzo kikuu, Mayweather (47-0, 26 KO). Hajapoteza hata pambano moja
katika hayo 47 na ameshinda 26 kwa KO huku akitamba Pacquiao atakuwa mtu wa 48
kumchapa.
Kwa
Pacquiao rekodi ni (57-5-2, 38 KO). Utaona Mfilipino huyo ameishapoteza
mapambano matano na sare mbili, lakini bado haitishi kumshusha.
Pacquiao
amecheza mechi nyingi zaidi ya Maywether, ana sare nyingi zaidi, ameshinda
nyingi zaidi hali kadhalika ana idadi kubwa zaidi ya sare na kupoteza.
Aina
ya upiganaji:
Hii
ni sehemu ya pili kwa ukubwa inayowavutia wengi kuona wawili hao wanapigana
tena. Kasi yao, mbinu na vipawa vya hali ya juu katika upiganaji.
Mayweather
anaaminika ndiye bondia mwenye uwezo mkubwa zaidi wa kujilinda dhidi ya wengine
wote duniani, lakini Pacquiao ndiye anayesifika kwa kutegua mitego mingi zaidi,
hapo ndiyo patamu.
Haukujua hili:
Kesho
Jumanne, Mayweather anatimiza miaka 38, hivyo atacheza pambano hilo akiwa
anamzidi Paquiao miaka miwili, kwa kuwa ana 36.
Kikubwa
zaidi ambacho haukujua, promota aliyemtoa Mayweather aitwaye Bob Arum, sasa
ndiye promota wa Pacquiao baada ya kukorofishana na bondia huyo mwaka 2006.
Mayweather
alianza kucheza ngumi za kulipwa mwaka 1996 baada ya kung’ara katika Olimpiki,
akachukuliwa na Bob Arum kabla ya kukorofishana miaka 10 baadaye. Hivyo
ushindani ndani hadi nye ya ulingo ni mkubwa.
Tiketi:
Umeambiwa
ni pambano ghali, hivyo lazima tiketi ziwe ghali na kweli ‘hazishikiki’.
Tiketi
ya bei rahisi imeelezwa kuwa dola 5,000 (Sh milioni 8.5) wakati zile
zinazozunguka ulingo zimepaa hadi kufikia dola 26,500 (zaidi ya Sh milioni 45),
kama unaishi Bongo, chagua ukaone pambano hilo ‘live’ au ununue Toyota IST zako
tano zote ufanye teksi!
0 COMMENTS:
Post a Comment