February 23, 2015


Pamoja na Yanga kuendeleza wimbi la ushindi katika michezo yake, nahodha wa timu hiyo, Nadir Haroub ‘Cannavaro’, bado ameendelea kumfikiria mshambuliaji wa BDF XI ya Botswana, Kobelo Seakanyeng kwa kuwa alimpa wakati gumu kwenye mchezo wa awali.


Yanga ambayo ilifanikiwa kuibuka na ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya timu hiyo katika mchezo wa kwanza wa Kombe la Shirikisho dhidi ya Waswana hao jijini Dar, Ijumaa hii itarudiana nao nchini kwao na Cannavaro bado anamfikiria straika huyo.

Cannavaro amesema kuwa licha ya ushindi walioupata katika mchezo wa awali, bado amekuwa akifikiria namna ya kumkaba straika huyo ambaye alimsumbua kwenye mchezo wa kwanza.

“Kazi kubwa bado ipo nchini Botswana kwa sababu jamaa wapo sawa, kuna yule straika wao aliyekuwa amevaa jezi namba saba halafu amenyoa kipara, ni mjanja halafu alikuwa anasumbua.


“Unajua amenipa muda wa kufikiria jinsi ya kumthibiti katika mchezo wa marudiano  pamoja na kucheza kwa tahadhari kubwa kwa sababu tunaenda kucheza ugenini na kwa jinsi alivyocheza hapa, mbele ya mashabiki wao atakuwa hatari zaidi kwetu,” alisema Cannavaro.

Yanga wanatarajia kuifuata BDF keshokutwa Jumatano, wakiwa na timu ya watu 37.

Katibu Mkuu wa Yanga, Jonas Kiboroha, amesema kati ya watu hao, 25 watakuwa ni wachezaji  huku viongozi na benchi la ufundi jumla wakiwa 12.

 “Mchezo wetu utachezwa saa kumi na moja jioni siku ya Ijumaa na tumejiandaa kuona tunafanikiwa kushinda mchezo huo na kujiweka katika nafasi nzuri ya kuendelea kusonga mbele,” alisema Kiboroha.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic