Kocha Mkuu wa Simba, Mserbia, Goran Kopunovic,
amemtaka kipa Hussein Shariff ‘Casillas’ kuhakikisha anakuwa fiti wakati
anajiunga na kikosi chake.
Kipa huyo, alijiunga na Simba katika usajili
wa mwanzoni mwa msimu huu akitokea Mtibwa Sugar.
Alisaini mkataba wa miaka
miwili lakini amekuwa akikumbwa na majeraha ya mara kwa mara.
Katibu Mkuu wa Simba, Stephene Ally, alisema
kocha huyo hana shida na kipa huyo, kikubwa anamtaka awe fiti kabisa kabla
hajaingia kwenye kikosi cha kwanza.
“Kopunovic
yupo tayari kufanya kazi na Casillas, lakini kocha ametoa sharti kwamba kama kipa
huyo anataka kurejea kikosini, basi awe amepona kabisa na fiti kwa ajili ya
ligi kuu.
“Kikubwa kocha anataka kuwa na mchezaji ambaye
yupo fiti, siyo majeruhi. Ni kama ilivyokuwa kwa Owino (Joseph) ambaye alipona
kabisa ndiyo akamrejesha kikosini,” alisema Stephene.
Kocha huyo, hivi karibuni alitangaza kuwa hana
kipa namba moja kwenye kikosi chake, kati ya Ivo Mapunda, Peter Manyika na
Casillas mwenyewe.
0 COMMENTS:
Post a Comment