![]() |
UONGOZI
wa Klabu ya Simba umemtangaza Haji Sunday Manara kuwa ofisa habari mpya kwenye klabu
hiyo inayoshiriki Ligi Kuu Bara.
Katibu
Mkuu wa Simba, Stephene Ally alisema kuwa ofisa habari huyo ameteuliwa na
kamati ya utendaji baada ya kuona anakidhi vigezo.
Stephene
amesema, aliyekuwa ofisa wa timu hiyo, Humphrey Nyasio yeye amebadilishiwa
majukumu katika sekretarieti ya Simba katika kuhakikisha wanafikia malengo yao.
“Uongozi
kwa jumla umelipitisha jina la Manara kuwa ofisa habari wetu katika klabu yetu
ya Simba na Nyasio aliyekuwa ofisa habari yetu tumembadilishia majukumu mengine,”
alisema Stephene.
.jpg)








0 COMMENTS:
Post a Comment