Kiungo mshambuliaji wa Yanga, Andrey Coutinho,
juzi Jumatano alishindwa kujizuia na kujikuta akimwaga chozi mara baada ya
kupewa taarifa ya kuikosa mechi dhidi ya Simba.
Mbrazili huyo alifanyiwa vipimo kwenye
Hospitali ya Muhimbili jijini Dar es Salaam na baada ya hapo ndipo akapewa
taarifa hizo ambapo anasumbuliwa na maumivu ya goti aliyopata wakati timu hiyo
ilipovaa na Mbeya City katika mechi ya Ligi Kuu Bara dhidi ya Prisons.
Coutinho alisema kuwa bora angekosa mechi zote
lakini siyo dhidi ya Simba yenye upinzani mkubwa.
“Ninaumia sana kuikosa mechi dhidi ya Simba,
kauli iliyotolewa na madaktari leo (Jumatano) mara baada ya kufanyiwa vipimo
imenifanya nikose furaha,” alisema Coutinho.
Aidha, Coutinho aliongeza kuwa, anaamini kikosi
chake kipo fiti na wachezaji wenzake lazima watawafunga Simba kutokana na jinsi
walivyo fiti kwa sasa.
0 COMMENTS:
Post a Comment