Klabu ya Al-Sadd ya Qatar imekanusha uzushi kwa kiungo Xavi harnandez amekamilisha uhamisho wa kujiunga nayo.
Uongozi
wa klabu hiyo umesema taarifa zinazosambaa kwamba Xavi anajiunga na klabu hiyo
na tayari ameingia mkataba ni uzushi mtupu.
Umeeleza
kwamba alikuwa nchini Qatar kwa ajili ya kuangalia mazingira ya eneo hilo akiwa
na familia yake.
Imeelezwa
kwamba Xavi alilazimika kwenda Doha akiwa na familia yake kuangalia kama
inaweza kuishi pale angalau kwa mwaka mmoja.
Lakini utata
ulianza baada ya Meneja mkuu wa mklabu hiyo, Abdulla Al-Berik,kutupia mtandaoni
picha ya Xavi na kusema ameishajiunga na klabu hiyo.
Huku
kukiwa na picha, meneja huyo alianzika maneno haya: “Tumefanikiwa kumsajili
Xavi na hii ndiyo picha yake akiwa na Mkurugenzi wetu Mtendaji, Muhammed
Ghoulam".
Hata
hivyo klabu hiyo imeendelea kusisitiza kwamba kweli iko katika majadiliano
ikijaribu kumshawishi Xavi kujiunga nayo ili amalizie soka lake katika klabu
hiyo.
0 COMMENTS:
Post a Comment