Liverpool ikiwa ugenini imeifunga Swansea kwa
bao 1-0 katika mchezo wa Ligi Kuu England.
Bao pekee la Liverpool limefungwa na nahodha
wake msaidizi Jordan Henderson kwa shuti lililomshika kipa wa Swansea.
Wenyeji Swansea walitawala kipindi cha kwanza
lakini wakashindwa kuzitumia nafasi kadhaa walizopata.
Liverpool wakacheza vizuri zaidi kipindi cha
pili huku wakionekana wametulia zaidi baada ya nahodha wao Steven Gerrard
kuingia.







0 COMMENTS:
Post a Comment