Polisi wa England wamemata kijana kwenye umri wa
miaka 15 kutokana na kutupia mtandaoni maandishi yanayolenga ubaguzi wa rangi.
Taarifa zinaelza maneno hayo ya kibaguzi,
yanamlenga mshambuliaji wa Arsenal, Danny Welbeck aliyefunga bao la ushindi wakati
Man United ikilala kwa mabao 2-1 katika michuano ya Kombe la FA.
Kijana huyo ametupia maneno kupitia mtandao wa
kijamii wa Twitter na Polisi wamesema wanaendelea na uchnguzi na kijana huyo
kaachiwa kwa dhamana hadi Aprili 13, atakapoitwa kwa ajili ya kesi hiyo
kuendelea kusikilizwa.
Mmoja wa maofisa wa Polisi wa Greater Manchester
amesema wameanza kufanya uchunguzi huo wa maneno hayo ya kibaguzi kwenye
mtandao wa Twitter.









0 COMMENTS:
Post a Comment