Kocha Mkuu wa AFC Leopards ya Kenya, Zdravko
Logarusic amesema anahitaji kubeba ubingwa.
Loga amesema angependa kubeba makombe akiwa
nchini humo kama alivyofanya katika timu yake ya zamani ya Gor Mahia.
Kocha huyo aliyewahi kuinoa Simba kabla ya
kufukuzwa amesema anajua kutakuwa na ugumu lakini anataka makombe na
ameishajiandaa.
“Haitakuwa kazi lahisi, ligi ya Kenya ina
ushindani sana. Lakini nataka makombe kwa Leopards,” alisema.
Loga amesema anakiamini kikosi chake ingawa
ni mwanzo lakini amekuwa akiwaambia wachezaji wake kuwa lazima wabebe makombe.







0 COMMENTS:
Post a Comment