Kikao cha Kamati ya Uendeshaji na Usimamizi wa Bodi ya Ligi Kuu
Tanzania imewapiga faini wachezaji kadhaa kutokana na makosa mbalimbali.
Kikao hicho kilichoketi jumanne ya tarehe 24, Machi 2015 jijini Dar es
salaam, kimepitia taarifa mbalimbali za michezo iliyochezwa na kutoa adhabu kwa
wachezaji na vilabu vya Ligi Kuu ya Vodacom.
Mchezaji Haruna Niyonzima wa
Yanga amepigwa faini ya sh. 500,000 (laki tano) kwa mujibu wa Kanuni ya 37(f)
kwa kupiga teke meza ya mwamuzi
wa akiba baada ya kutolewa nje kwa kadi nyekundu. Suala la mshambuliaji wa
Yanga Amissi Tambwe kumshika korodani beki wa Simba SC Murshid Juuko
limepelekwa kwenye Kamati ya Nidhamu.
Naye
mshambualiji wake Dany Mrwanda akipigwa faini ya sh. 500,000 kwa mujibu wa
Kanuni ya 14(12) kwa kutopeana mikono na wachezaji wa timu hiyo.
Kipa wa timu ya Simba SC, Ivo
Mapunda amepewa onyo kwa kufunika tangazo la mdhamini wa Ligi
Kuu (Vodacom) kwa kutumia taulo lake wakati wa mechi dhidi ya Yanga, hatua
kali za kinidhamu zitachukuliwa dhidi yake iwapo atarudia kufanya tukio la aina
hiyo.
Pia kiungo Salum Abubakar wa
Azam FC na Richard Maranya wa JKT Ruvu wamepigwa faini ya sh. 500,000 (laki
tano) kila mmoja na kusimamishwa mechi tatu kwa mujibu wa Kanuni ya 37(3) kwa
kupigana uwanjani kwenye mechi namba 123 ambapo walitolewa nje kwa kadi
nyekundu.
Klabu ya Kagera Sugar imepigwa
faini ya sh. 300,000 (laki tatu) kwa mujibu wa Kanuni ya 14(9) baada ya timu
yake kugoma kuingia kwenye vyumba vya kubadilishia nguo kwenye mchezo namba 130
dhidi ya Young Africans uliofanyika kwenye Uwanja wa Taifa.
0 COMMENTS:
Post a Comment