STAND UNITED. |
Kikao cha Kamati ya Uendeshaji na Usimamizi wa Bodi ya Ligi Kuu
Tanzania kilichoketi jumanne ya tarehe 24, Machi 2015 jijini Dar es
salaam, kimepitia taarifa mbalimbali za michezo iliyochezwa na kutoa adhabu kwa
wachezaji na vilabu vya Ligi Kuu ya Vodacom.
Katika mechi namba 107
iliyowakutanisha wenyeji Ndanda FC dhidi ya Coastal Unioni, klabu ya Ndanda
imepigwa faini ya sh. 500,000 (laki tano) kwa mujibu wa Kanuni ya 42(1) ya Ligi
Kuu ya Vodacom kutokana na
washabiki wake kumrushia chupa za maji mwamuzi msaidizi Anold Bugado.
Mechi namba 108 iliyochezwa
Uwanja wa Kambarage mjini Shinyanga, (Stand United dhidi Simba SC), wenyeji
timu ya Stand United imepigwa faini ya sh. 300,000 (laki tatu) kwa mujibu wa
Kanuni ya 14(8) kutokana na timu yake kuchelewa kufika uwanjani kwa dakika
ishirini.
Mechi namba 132
iliyozikutanisha Azam na Ndanda SC kwenye uwanja wa Chamazi, klabu ya Ndanda
imepigwa faini ya sh. 500,000 (laki tano) kwa mujibu wa Kanuni ya 42(1) baada
ya washabiki wake kuwamwagia maji na kuwarushia chupa za maji washabiki wa
Azam.
Aidha klabu ya Stand United
imepigwa faini ya sh. 300,000 (laki tatu) kwa mujibu wa Kanuni ya 14(8) kwa
kuchelewa kufika uwanjani kwenye mechi namba 134 dhidi ya timu ya Mbeya
City, pia imepigwa faini ya
sh. 500,000 (laki tano) kwa mujibu wa Kanuni ya 14(9) kwa kutoingia kwenye
vyumba vya kubadilishia nguo kwenye mchezo huo.
Kiongozi wa Stand United,
Muhibu Kanu amepelekwa kwenye Kamati ya Nidhamu baada ya kuondolewa kwenye
benchi na mwamuzi wa mchezo dhidi ya Mbeya City kutokana na kutumia lugha ya
kuhamasisha vurugu kwa timu yake na kupinga uamuzi wa refarii.
Katika mchezo namba 135
uliochezwa jijini Tanga na kuwakutanisha wenyeji Mgambo Shooting dhidi ya Yanga
SC, Yanga SC imepigwa faini ya sh. 500,000 (laki tano) kwa mujibu wa Kanuni ya
42(1) kutokana na washabiki wake kuvamia uwanja baada ya mechi namba 135 dhidi
ya Mgambo Shooting kwenye Uwanja wa Mkwakwani.
0 COMMENTS:
Post a Comment