April 8, 2015


Yanga imetoa onyo sasa kwamba haitaki utani baada ya kuichapa Coastal Union kwa mabao 8-0.

Katika mchezo huo wa Ligi Kuu Bara kwenye Uwanja wa Taifa, Dar, leo. Yanga ilionyesha imepania ushindi baada ya kwenda mapumziko ikiwa inaongoza kwa mabao matatu.

Kipindi cha pili kilikuwa na mabao mengine matano na Amissi Tambwe alifanikiwa kufunga mabao manne, Simon Msuva, Salum Telela na Mliberia Kpaj Sherman akaona mwezi kwa kucheka na nyavu
Yanga imezidi kujichimbia kileleni baada ya kufikisha pointi 43.

Azam FC yenye inabaki katika nafasi ya pili baada ya sare ya bao 1-1 dhidi ya Mbeya City kwenye Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, Dar.


Sare hiyo imeifanya Azam FC kufikisha pointi 37 lakini ina  mchezo mmoja pungufu kwa Yanga.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic