Kocha Mkuu wa Chelsea, Jose Mourinho amesema kikubwa anachokitaka
ni pointi na si kutawala au kukaa na mpira muda mrefu.
Mourinho amesema kikubwa anachoangalia ni ushindi kwa kuwa Chelsea
inahitaji pointi tatu kuliko kipingidi kingine chochote.
Chelsea iliyo kileleni mwa Ligi Kuu England imeongeza pendo lake
la pointi hadi kufikia 10 dhidi ya Arsenal iliyo nafasi ya pili baada ya
kufanikiwa kuidunda Man United kwa bao 1-0.
Hata hivyo, wageni man United walitawala mchezo na Chelsea
ikamiliki kwa mpira kwa asilimia 29 tu.
“Sisi tunataka pointi tatu, si kumiliki mpira,” alisisitiza
Mourinho raia wa Ureno.
0 COMMENTS:
Post a Comment