Azam FC imefanikiwa kukata tiketi ya kucheza Kombe la Shirikisho msimu ujao.
Azam imepata nafasi hiyo baada ya kuifunga Yanga kwa mabao 2-1 katika mechi ya Ligi Kuu Bara leo kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar.
Baada ya ushindi huo, maana yake Azam FC imefikisha pointi 48 ambazo haziwezi kufikiwa na Simba ambayo sasa ina pointi 44 ikiwa imebakiza mechi moja.
Hata kama itashinda, maana yake itafikisha pointi 47 na kwa msimu mwingine, Simba inakosa tena ushiriki wa michuano ya kimataifa.
Nilichoka kuona mashabiki wa Yanga walipokuwa wanashangilia bao la Azam.
ReplyDelete