Kocha ‘mpya’ wa Azam FC, Stewart Hall anaratajia kuanza kazi anatarajia
kuanza Juni 15, mwaka huu.
Hall anayereja Azam FC kwa mara ya tatu ndani ya
kipindi cha miaka sita, ameingia mkataba wa miaka miwili kuinoa Azam Fc.
Msemaji wa Azam FC, Jaffar Idd Maganga amethibitisha
kuhusiana na hilo na kusema atasaidiwa na kocha wa makipa kutoka England.
“Ataanza kazi tarehe 15 mwezi ujao, kwa sasa unaweza
kusema tayari ni kocha wa Azam FC,” alisema.
“Tumeingia naye mkataba wa miaka miwili, tunaaamini
atakuwa msaada mkubwa kwa kuwa tayari anaijua Azam FC na nini inataka.”
Huo unakuwa mkataba wa tatu Hall raia wa Uingereza
anaingia na timu hiyo waliokuwa mabingwa wa Tanzania kabla ya kuvuliwa ubingwa
huo msimu uliopita na Yanga ya Dar es Salaam.
0 COMMENTS:
Post a Comment