WAKATI WA UHAI WAKE, SHEIKH OMARY. |
Mwenyekiti mpya wa Villa Squad, Sheikh Omar Alhady
amefariki dunia katika Hospital ya Taifa ya Muhimbili.
Taarifa zilizotolewa na uongozi wa klabu hiyo yenye
makao yake makuu Magomeni jijini Dar es Salaam zimeeleza marehemu alikwua
akisumbuliwa na tatizo la figo.
SHEIKH OMARY (WA TATU KULIA) AKIWA NA VIONGOZI WENGINE WA VILLA, GODIGODI (KULIA), IDD MOSHI ANAYEMFUATIA NA VIONGOZI WENGINE. |
Sheikh Omary alichaguliwa kuwa mwenyekiti katika
mkutano mkuu wa wanachama uliofanyika Mei 17, maana yake amekaa madarakani kwa
siku kumi tu.
Enzi za uhai wake Sheikh Omary alikuwa ni mmoja wa
masheikh mashuhuri nchini pia alikua ni Imàm katika msikiti wa Kichangani jijini
Dar es Salaam.
IMETOLEWA NA BOSI WA MAWASILIANO WA VILLA SQUAD, IDDI
GODIGODI.
0 COMMENTS:
Post a Comment