May 1, 2015

MALINZI
Rais wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Jamal Malinzi amewatakia kila la kheri wawakilishi pekee wa Tanzania katika Kombe la Shirikisho Barani Afrika (CC) timu Young Africans katika mchezo wake wa marudiano dhidi ya timu ya Etoile du Sahel utakaochezwa kesho nchini Tunisia.


Katika salamu zake Malinzi amesema ,Young Africans wakiwa ndio timu wawakilishi pekee wa Tanzania na Afrika Mashariki katika michuano ya kimataifa barani Afrika wanapaswa kupambana kuhakikisha wanasonga mbele katia hatua inayofuata.

Katika mchezo wa awali uliofanyika wiki mbili zilizopita jijini Dar es salaam, Young Africans ilitoka sare ya bao 1- 1 na Etoile du Sahel, na mshindi wa jumla kwa mchezo wa huo, atacheza hatua ya mtoano (Play-off) dhidi ya timu zitakazokuwa zimetolewa kwenye Ligi ya Mabingwa (CL) kuwania kufuzu kwa hatua ya makundi.

Mchezo huo wa marudiano utapigwa kesho jumamosi katika dimba la Olympique de Sousse katika mji wa Sousse kuanzia majra ya saa 3 kamili usiku kwa saa za Afrika Mashariki na Kati

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic