May 1, 2015


Utamu wa Ligi Kuu ya Bara unatarajiwa kuendelea wikiendi hii lakini kivutio kikubwa kikiwa ni mjini Mbeya.

Jumamosi katika Uwanja wa Sokoine wapinzani wa jiji la Mbeya, Prisons FC watakua wenyeji wa wagonga nyundo Mbeya City mchezo utaochezwa majira ya saa 10 kamili kwa saa za Afrika mashariki na Kati.

Katika Uwanja wa Nangwanda Sijaona wenyeji timu ya Ndanda SC watawakaribisha wakata miwa wa Kagera Sugar, huku jijini Tanga Mgambo Shooting wakiwa wenyeji wa maafande wa JKT Ruvu mchezo utakaopigwa kwenye Uwanja wa Mkwakwani.
 
PRISONS
Jumapili katika uwanja wa Taifa jijini Dar es salaa, Simba SC watawakaribisha Azam FC, mchezo ambao unatabiriwa kuwa na upinzani mkali kusaka nafasi ya pili ili mwakani kuweza kuwakilisha Tanzania katika michuano ya Kombe la Shirikisho barani Afrika.


Jijini Tanga wagosi wa kaya Coastal Union watawakaribisha timu ya Stand United kutoka mjini Shinyanga, mchezo utakaochezwa kwenye uwanja wa Mkwakwani, huku kwenye Uwanja wa Manungu mjini Morogoro wenyeji Mtibwa Sugar wakiwakaribisha maafande wa Ruvu Shooting.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic