Utamu wa Ligi Kuu Bara kwa
mabingwa kupigiwa makofi wakitoka vyumbani umefanyika leo.
Wachezaji wa Azam FC waliokuwa
mabingwa watetetzi wamewapigia makofi wachezaji na memba wa benchi la ufundi la
Yanga ambao ni mabingwa wapya.
Tukio hilo lilitokea wakati
Yanga wakiingia uwanjani katika mechi yao ya Ligi Kuu Bara dhidi ya Azam FC
kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar.
Utaratibu huo umekuwa ukitumika
zaidi kwenye Ligi Kuu England na safari hii umetumika Tanzania Bara kwa bingwa
kupigiwa makofi kama anakuwa amebaki mchezo au michezo baada ya kuwa
ameishabeba ubingwa.
0 COMMENTS:
Post a Comment