Aliyewahi kuwa mlezi wa
Simba, Rahma Al Kharoos, maarufu kama Malkia wa Nyuki, amekutana na masaibu
baada ya akaunti yake ya email ‘kutekwa’ na kuanza kutumika vibaya.
Akaunti yake ‘ilitekwa’ na
wahalifu wa mtandaoni raia wa Nigeria na ikaanza kutumiwa kuwaomba fedha watu
mbalimbali kutoka sehemu tofauti duniani.
Wahalifu hao walikuwa
wakiwaomba fedha watu kadhaa waliowasiliana nao kwa madai wao ndiyo Malkia wa Nyuki,
wako safarini barani Ulaya wamekwama kifedha.
Akizungumza kutoka Muscat, Oman, Malkia wa Nyuki alikiri kutokea kwa jambo hilo
lakini akasisitiza ni wahalifu raia wa Nigeria ndiyo waliokuwa wakifanya hivyo.
“Hakika sikuwa mimi, hao
watu waliichukua akaunti yangu. Kwa kweli sijui wanaingiaje na mwisho wakaanza
kuwasiliana na watu kadhaa.
“Walikuwa wakifanya hivyo
lakini uzuri watu wengi waliweza kuwasiliana na mimi na kunieleza nikalifanyia
kazi,” alisema.
Wizi wa kimtandao umekuwa
ukikua kila kukicha huku raia wa Nigeria ndiyo wakionekana kuwa namba moja
katika utapeli huo.
Hata hivyo, Malkia wa Nyuki
alisisitiza kwamba hakukuwa na madhara makubwa na alikuwa katika harakati ya
kuikomboa anuani yake hiyo ya email.
0 COMMENTS:
Post a Comment