Mashabiki wa Yanga sasa roho kwatu
baada ya leo kutambulishwa mshambuliaji wao mpya, Donald Ngoma.
Mashabiki hao wamemuona Ngoma raia wa
Zimbabwe baada ya kuwasili na kupelekwa kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es
Salaam ambako Yanga ilikuwa inaivaa SC Villa ya Uganda katika mechi yao ya
kirafiki.
Ngoma alitua uwanjani hapo akifuatana
na baadhi ya viongozi na wanachama wa Yanga.
Pia kiungo mkabaji mwenye uwezo wa
kucheza beki, Joseph Tetteh Zutah raia wa Ghana ni kati ya waliotua leo kwa ajili ya
kumalizana na Yanga.
Ngoma aliwasalimia mashabiki wa Yanga
ambao walishangilia kwa nguvu huku wakitumia muda huo kuwabeza wenzao wa Simba
walionekana kuwa kimya.
0 COMMENTS:
Post a Comment