July 8, 2015


Zikiwa zimebaki siku tisa kabla ya kuanza kwa michuano ya Kombe la Kagame, mshambuliaji wa Azam FC, Mrundi, Didier Kavumbagu, amesema anatamani kukutana na timu bora katika michuano hiyo, hasa Yanga ili kupima uwezo wake na ubora wa kikosi chao.


Yanga na Azam ndizo timu zinazoiwakilisha Tanzania Bara katika michuano hiyo ambapo bingwa huchota kitita cha dola 30,000 (Sh milioni 60 kwa sasa) za Kimarekani.

Azam wamepata nafasi hiyo wakiwa mabingwa wa Ligi Kuu Bara, huku Yanga wakiwa wenyeji wa michuano hiyo kwa kuwa walishika nafasi ya pili.

Kavumbagu amesema mchezaji kujua uwezo wako ni lazima kukutana na timu yenye ubora.

“Maandalizi yanakwenda vizuri, tumejipanga kukutana na upinzani kwa sababu mashindano yanahusisha mabingwa wa nchi, hivyo kila timu ni bora. Ili kufanya vizuri, tunahitaji kuwa na juhudi za ziada.


“Ninajua Yanga ni timu bora, ninatamani sana kukutana nayo ili kupata changamoto. Unajua ili mchezaji au timu kujua mpo imara kiasi gani, ni lazima mkutane na timu bora, hapo ndipo mtajua mna timu ya aina gani. Binafsi ninapenda sana kukutana na timu za aina hiyo ikiwemo Yanga yenyewe,” alisema Kavumbagu ambaye msimu uliopita alifunga mabao 10 katika Ligi Kuu Bara.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic