Uongozi wa Azam FC
umesema hauna tatizo na uamuzi wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF)
kumbadilisha mwamuzi wa mchezaji wa Ngao ya Jamii, Jumamosi.
Mchezaji huo unawakutanisha
Azam FC dhidi ya Yanga ambao utarushwa moja kwa moja na runinga ya Azam TV,
sasa utachezeshwa na Martin Saanya.
TFF imembadilisha Israel
Nkongo ambaye ameelezwa kuwa na matatizo ya misuli.
Katibu wa Azam FC,
Idrissa Nassor amesema wao wanachotaka ni uchezeshaji wa kufuata sheria 17 za
soka.
“Kwa kweli hatuna
tatizo, kama sheria 17 za soka zitafuatwa sisi hatuna tatizo.
“Hiyo si kazi yetu,
kikubwa ni maandalizi ambayo tumekuwa tukiendelea kuyafanya,” alisema Nassor.
0 COMMENTS:
Post a Comment