Timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) inayodhaminiwa
na bia ya Kilimanjaro sasa itaondoka nchini siku ya jumapili usiku kuelekea
Istambul nchini Uturuki kwa kambi ya siku nane kujiandaa na mchezo dhidi ya
Nigeria Septemba 05, 2015.
Stars inatarajiwa kuondoka jumapili usiku na shirika
la ndege la Uturuki (Turkish Airlines) na kuwasili Istambul (Ataturk Airport)
siku ya jumatatu majira ya saa 5 kamili asubuhi, kisha kuelekea Kocael katika
hoteli ya Green Park Kartepe ambapo ndio itakua kambi yake ya wiki moja.
0 COMMENTS:
Post a Comment