Azam FC imemuongezea Serge Wawa mkataba wa
mwaka mmoja.
Zoezi hilo limefanyika leo jijini Dar es
Salaam baada ya wakala wa Wawa kuwasili nchini leo.
Ofisa Mtendaji Mkuu wa Azam FC, Saad Kawemba
amethibitisha kuhusiana na hilo.
“Ni jukumu letu kufanya hivyo, lakini mwalimu
pia alikuwa anamhitaji,” alisema Kawemba.
Wawa raia wa Ivory Coast alionyesha uwezo
mkubwa katika Ligi Kuu Bara na baadaye
michuano ya Kagame ambayo Azam FC imeibuka bingwa bila ya kufungwa hata bao
moja.
0 COMMENTS:
Post a Comment