Mshambuliaji wa Simba, Elius Maguri ameingia
kwenye hofu kubwa ya kutemwa.
Taarifa za ndani ya Simba zimeeleza uongozi wa
Simba umeamua kumtema.
Lakini taarifa nyingine zimeeleza kwamba Simba
iko tayari kumtoa mkopo na imeishazitaarifu baadhi ya timu zinazomtaka.
Akizungumza na SALEHJEMBE, Maguri amesema bado
hajapewa taarifa rasmi na uongozi wa Simba, lakini dalili ya mvua ni mawingu.
“Nimeondolewa kwenye kambi kwa kwa ajili ya
Simba Day.
“Kidogo imenishangaza kwa kuwa ni siku ambayo
wachezaji wanapaswa kutambulishwa kwa wanachama na mashabiki.
“Kama sitambulishwi siku hiyo, maana yake siko
kwenye hesabu za klabu. Lakini hakuna kiongozi aliyeniambia.
“Inaniumiza sana, hasa ukizingatia nimeachwa
siku ya mwisho baada ya kufanya mazoezi kwa kujituma sana Zanzibar.
“Ajabu kuna timu ikiwemo Ndanda ya Mtwara
zinanipigia zikitaka nijiunge nazo kwa kuwa uongozi wa Simba umezieleza kuwa
zinichukue,” alisema Maguri akionekana kusononeka.
0 COMMENTS:
Post a Comment