Mwenyekiti wa Yanga, Yusuf manji amerudishwa
katika nafasi yake ya kuwania udiwani katika kata ya Mbagala Kuu.
Manji alishinda kwa kishindo, lakini
akaenguliwa katika hali iliyoelezwa kuwa ya figisufigisu.
Hata hivyo, KAmati Kuu ya Chama Cha
Mapinduzi iliyokaa jana, imemrejesha Manji baada ya wahusika kukimbia wakati wa
kuhojiwa.
“Ulipofika wakati wa wahusika kuhojiwa,
hawakuwepo, walipopigiwa simu walikuwa wamechelewa na kusema wanakuja lakini
baada ya muda walizima simu.
“Hali hiyo ilifanya kamati kuu moja kwa moja
kuchukua uamuzi wa kumrejesha Manji katika nafasi yake aliyoshinda kwa
kishindo,” kilieleza chanzo.
Wananchi wa Mbagala Kuu walionyesha hasira
zao kwa kuvamia makao makuu ya CCM Mkoa wa Dar es Salaam wakitaka Manji
arudishwe baada ya kugundua aliondolewa kwa fitita licha ya ushindi wake wa
kishindo.
0 COMMENTS:
Post a Comment