Mkuu wa kitengo cha habari cha Yanga, Jerry
Muro amewakaribisha watani wao Simba akiwataka wajitokeze kwa wingi katika
mechi ya Ngao ya Jamii kwenye Uwanja wa Taifa Jumamosi.
Mechi hiyo inawakutanisha Yanga dhidi ya
Azam FC na Muro amesisitiza kwamba ni mechi ya “Wa kimataifa”.
“Ni mechi nzuri na itakuwa ngumu, tuna
uhakika wa kushinda. Kikubwa pia tunawakaribisha ndugu zetu Simba, acha nao
waje.
“Waje waone wakimataifa wakipambana,
wasijisikie vibaya kuja kuona. Hawana nafasi ya kuona mechi nzuri kama hiyo
hata kama wao si wakimataifa,” alijinadi Muro.
Utani wa Simba na Yanga ulianza tokea mwaka
1936 baada ya kuanzishwa rasmi kwa Simaba ikitokea kwenye ubavu wa Yanga.
0 COMMENTS:
Post a Comment