Najua uliwahi kuisikia ile stori ya Steve Yanga kumwaga chozi baada ya Yanga kutundikwa mabao 5-0 na Simba, kuanzia bapo akawa maarufu.
Sasa Steve amehamia Azam
FC ambao ndiyo mabingwa wa Kombe la Kagame.
Lakini stori nyingine
tamu ya kuvutia ni ya kijana Louis Diamond mwenye umri wa miaka mitano ambaye
alimwaga chozi baada ya kuona mshambuliaji Robin van Persie akihama Manchester
United na kujiunga na Fenerbahce ya Uturuki.
Picha za video za
Diamond akilia zilisambaa kwa kasi kubwa mtandaoni na wengi walionekana
kumuonea huruma.
Kutokana na hali hiyo,
uongozi wa Fenerbahce uliamua kumpa nafasi Diamond ambaye ni shabiki wa kutupwa
wa Manchester United pamoja na familia yake kutembelea Uturuki ili apate nafasi
ya kumuona van Persie ambaye ni shujaa wake.
Diamond amepewa ofa ya
kukaa Istambul kwa siku tano akiwa katika hoteli bomba kabisa, akiwa na wazazi
wake watamuona van Persie ikiwa ni pamoja na kupata nafasi nyingine ya kuona
mechi ya ufunguzi wa Ligi Kuu Uturuki, van Persie akiwa uwanjani anaichezea Fenerbahce.
VAN PERSIE AKIWA KAZINI UTURUKI |
0 COMMENTS:
Post a Comment