August 11, 2015


Kampuni ya simu za mikononi ya Vodacom imekubali kuongeza mkataba wa miaka mitatu kuendelea kuidhamini Ligi Kuu Bara.


Vodacom imeishakubaliana kimsingi na TFF na Bodi ya Ligi (TPLB) kwa ajili ya kuongeza mkataba mpya wa miaka mitatu.

Kabla ya hapo, Vodacom sasa imeidhamini ligi hiyo kwa miaka saba sasa.

“Kweli makubaliano yamefikiwa, kesho kutakuwa na shughuli ya kusainishana mkataba itakayofanyika pale Mlimani City,” alisema Nkulu.

Taarifa zinaeleza kwamba kuna maboresho makubwa ndani ya mkataba huo yamefanyika.


Ligi hiyo sasa ina timu 16 badala ya 14 kama ilivyokuwa imezoeleka.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic