Na Saleh Ally
Rais Jakaya Kikwete amesema ataendelea kuwa mlezi wa
wasanii hata baada ya kumaliza muda wake wa uongozi.
Kikwete ameyasema hayo katika hafla maalum ya kumuaga
iliyoandaliwa na Muungano wa Wasanii wa Tanzania waliokuwa wakimuaga na
kumshukuru kwa ushirikiano mkubwa wakati wa uongozi wake.
Katika hafla hiyo iliyofana kwenye Ukumbi wa Mlimani
City, Kikwete aliwaambia wasanii yuko tayari kuendelea kuwa mlezi wao.
“Nitaendelea kuwa mlezi, ningependa kuifanya kazi hii
baada ya kustaafu. Ninaamini nitakuwa bado ni mwananchi mwenye jina.
“Kama nitaingia sehemu na kupiga hodi, nikazungumzia
jambo fulani kuhusiana na wasanii, ninaamini nitasikilizwa.
“Hivyo nitaendelea kuwapigania kadiri ya uwezo wangu. Lakini
kabla ya Oktoba, nitajitahidi mambo kadhaa niyatimize kwa kuwa hadi sasa kuna
baadhi ambayo nimeishayatimiza kwa kushirikiana nanyi,” alisema Kikwete.
Wasanii mbalimbali walitumbuiza katika hafla na
Kikwete alikabidhiwa picha yenye sura yake ambayo ina majina ya wasanii
mbalimbali.
0 COMMENTS:
Post a Comment