Timu ya taifa ya Tanzania,
Taifa Stars, imezidi kushuka katika viwango vya ubora wa Shirikisho la Soka la
Kimataifa (Fifa) ambapo imeshuka kwa nafasi moja zaidi na sasa inashika nafasi
ya 140.
Orodha hiyo iliyotolewa
jana imeonyesha kuwa, Tanzania ndiyo nchi inayoshika nafasi ya chini zaidi
katika Ukanda wa Afrika Mashariki ambapo Uganda inashika nafasi ya 74, Kenya
ikiwa ya 116.
Algeria ndiyo inayoongoza
kwa Afrika kwa kuwa inashika nafasi ya 19 ikifuatiwa na Ivory Coast inayoshika
nafasi ya 21.
Timu zinazoongoza katika 10
bora ni; Argentina, Ubelgiji, Ujerumani, Colombia, Brazil, Ureno, Romania,
England, Wales na Chile.
0 COMMENTS:
Post a Comment