Simba iko katika hatua za mwisho
kumalizana na mshambuliaji hatari kutoka Senegal ambaye anatarajia kutua nchini
ndani ya siku mbili zijazo.
Mshambuliaji Papa Niang, raia wa Senegal
aliyezaliwa Desemba 5, 1988, sasa ana miaka 26 ametua jijini Dar es Salaam leo asubuhi.
Niang ambaye inaelezwa ni mdogo wa Mamadou
Niang, ametua jijini Dar es Salaam kumalizana na Simba na mara moja kuanza
kazi.
Akizungumza na SALEHJEMBE mara tu baada ya
kutua kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, Niang amesema yuko
tayari kufanya kazi.
“Nimekuja nikiwa tayari, inategemea
makubaliano yangu na klabu hii yatakuwaje,” alisema.
Taarifa zinaeleza kwamba kabla ya kumsajili, Simba itampa nafasi ya mazoezi ya siku tatu, pia ataichezea katika mechi ya kirafiki dhidi ya Mwadui FC.
0 COMMENTS:
Post a Comment