Timu ya
Mwadui FC ya mkoani Shinyanga, jana Jumapili ilifanikiwa kuifunga Friends
Rangers ya jijini Dar kwa mabao 2-1 katika mchezo wa kirafiki uliopigwa Uwanja
wa Karume, Dar.
Mabao ya
Mwadui yalifungwa na Fabian Gwise dakika ya 59 na Stima (75) huku lile la
kufutia machozi la Friends likiwekwa kimiani na Tegete (88). Kocha wa Mwadui,
Julio muda wote alikuwa akimtania, Herry Mzozo ambaye anainoa Friends kwa
kumuambia mechi hiyo ameroga kutokana na wachezaji wake kukosa mabao ya wazi
ambayo anaamini wangewafunga mengi tu.
0 COMMENTS:
Post a Comment