August 11, 2015


Yanga itashuka dimbani Jumapili kucheza mechi ya kirafiki dhidi ya Mbeya City.


Mechi hiyo itapigwa kwenye Uwanja wa Sokoine mjini Mbeya ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya Ligi Kuu Bara.

Yanga imeweka kambi mjini Tukuyu kujiandaa na ligi kuu, na tayari imeshacheza mechi moja ya kirafiki dhidi ya Kimondo ya Mbozi na kushinda kwa mabao 4-1.


Kabla ya mechi hiyo ya Jumapili, Yanga inatarajia kushuka dimbani kesho kucheza na Prisons ya Mbeya.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic