Mshambuliaji mpya wa Simba, Kelvin Ndayisenga
raia wa Burundi amesema anajiamini atakuwa msaada Simba.
Ndayidenga amefunga bao lake la kwanza jana wakati Simba ilipoivaa URA katika mechi ya kirafiki kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.
Ndayisenga ameiambia SALEHJEMBE kwamba kikosi
cha Simba kina mpangilio mzuri unaoweza kumpa nafasi ya kufanya vizuri.
“Simba ni timu nzuri na ina mpangilio bora,
nikibaki hapa ninaamini nitafanya vizuri.
“Mimi ninajiamini nitakuwa msaada mkubwa katika
kikosi cha Simba,” alisema.
0 COMMENTS:
Post a Comment