MAGURI AKIPAMBANA... |
Zikiwa zimepita siku kadhaa tangu aliyekuwa mshambuliaji wa Simba,
Elias Maguri aachwe ndani ya kikosi hicho, kocha wake, Muingereza, Dylan Kerr,
ametoboa siri iliyokuwa nyuma ya pazia la sakata hilo kwa kusema kuwa,
mshambuliaji huyo alimfuata akitaka kuondoka.
Maguri ambaye alitua Simba na kupewa mkataba wa miaka miwili
akitokea timu ya Ruvu Shooting, ameachwa ndani ya kikosi hicho baada ya uongozi
wa klabu hiyo kumsitishia mkataba wake ambapo kwa sasa ni mchezaji huru licha
ya kuripotiwa kwamba ana mipango ya kurejea kwenye timu yake ya zamani.
Kerr ambaye ni beki wa zamani wa kushoto wa timu ya Kilmarnock ya
Scotland, amesema alikubali kumruhusu mshambuliaji huyo kuondoka ndani ya
kikosi hicho kutokana na yeye kumfuata na kuomba ruhusa ya kuondoka kutokana na
kuona mambo yanakuwa mabaya kwake.
KERR |
“Maguri mwenyewe alinifuata na kuniambia juu ya suala lake hilo la
kutaka kuondoka, sikuwa na tatizo na sikuwa na sababu ya kumpinga kutokana na
nafasi yake kikosini kuwa ndogo, ukilinganisha na washambuliaji wengine
waliopo,” alisema Kerr ambaye ni shabiki mkubwa wa Manchester United ya
Uingereza.
Hivi karibuni, Maguri alikuwa akilalama kwamab hajui mustakabari
wake ndani ya kikosi cha Kerr baada ya kuondolewa siku moja kabla ya Simba Day.
0 COMMENTS:
Post a Comment