MAGURI |
Uongozi wa Simba, leo umetangaza rasmi kuachana ana mshambuliaji wake
Elius Maguri pamoja na kipa Ivo Mapunda.
Tayari SALEHJEMBE iliandika kuhusiana na kutemwa na Maguri, lakini
uongozi wa Simba umeweka hadharani.
Msemaji wa Simba, Haji Manara amesema Kocha Mkuu, Dylan Kerr ndiye
alitoa mapendekezo.
“Tunaheshimu mapendekezo ya kocha Kerr na sasa Maguri ni mchezaji huru
na tumemalizana vizuri sana,” alisema Manara.
Dalili za Maguri kuachwa Simba zilianza baada ya kuondolewa kwenye Simba
Day.
Hali hiyo ilionyesha kumshangaza, lakini uongozi wa Simba uliendelea
kuwa kimya hadi ulivyotangaza leo.
Kuhusiana na Ivo, yeye tayari alishapewa fedha za usajili. Lakini uongozi
wa Simba umemueleza kwamba hakuwa na ushirikiano wakati akitafutwa kusaini
mkataba.
Wakati fulani Ivo aliwahi kushutumu kuhusiana na vyombo vya habari kuwa
vinadai haonekani na anatafutwa kusaini mkataba jambo ambalo halikuwa kweli na
uzushi mtupu.
Lakini ndiyo jambo aliloelezwa na uongozi wa Simba leo, kwamba hakuwa na
ushirikiano, hivyo anaweza akaendelea na mambo yake.
0 COMMENTS:
Post a Comment