Kiungo mshambuliaji wa zamani wa Simba, Uhuru Selemani amewataka Watanzania kuondokana na uoga wa kujaribu na kuondoa hofu ya kuonekana wamefeli.
Uhuru
ambaye sasa anakipiga katika timu ya Royal Eagle alikopelekwa mkopo akitokea Jomo
Cosmos, zote za Afrika Kusini amesema uoga unawaumiza Watanzania wengi.
Akipiga stori na SALEHJEMBE kutoka jijini Durban, Uhuru, amesema uoga ni tatizo.
"Hofu ya wengi ni kufeli, tena wanajua baada ya kufeli magazeti yatawaandika sana kwamba hawakuwa na lolote au wameshindiwa.
"Lakini si vibaya kujaribu tena na tena, huwezi kujua timu unayofanya majaribio kocha anahitaji nini. Tena kama unaenda waambie haya ni majaribio yangu ya nne.
"Kwani hata timu ikiona umefanya majaribio mara nyingi wanajua unakubali, ni mtu unayetamaniwa na timu nyingi,” alisema.
Uhuru aliyewahi kuzichezea Coastal Union, Mtibwa Sugar na Simba amesema anaendelea kupambana licha ya ushindani mkubwa kisoka nchini humo.
0 COMMENTS:
Post a Comment