Baada ya kutembeza vipigo mkoani
Mbeya, Yanga imerejea jijini Dar es
Salaam na kuanza kambi.
Kambi hiyo ni maandalizi ya mwisho
kujiandaa na mechi ya Ngao ya Jamii dhidi ya Azam FC.
Yanga ilikuwa Mbeya ambako ilianza
mechi yake ya kwanza ya kirafiki dhidi ya Kimondo ya Mbozi na kuitwanga kwa
mabao 4-1.
Baada ya hapo ilikutana na Prisons na
kuchaopa mabao 2-0 kabla ya kuituliza Mbeya City kwa mabao 3-2.
Sasa Yanga imerejea kumalizia kambi
yake jijini Dar es Salaam kabla ya kuivaa Azam FC wikiendi hii.
0 COMMENTS:
Post a Comment