Mshambuliaji wa Mtibwa Sugar, Said Bahanuzi, ameibuka na kusema
wapinzani wao katika Ligi Kuu Bara wasitambe sana kwani watawaumbua kwa
kuwafunga kutokana na kuwa
na kikosi bora.
Bahanuzi aliyetupiwa virago na Yanga, amesema atapigana
kufa na kupona kuhakikisha anaisaidia timu yake kufanya vizuri katika michezo
yote ya ligi.
Alisema timu pinzani kwao kama Simba, Yanga na
Azam FC, zimekuwa na mazoea ya kusifu vikosi vyao wakati uwanjani hucheza soka
la kawaida sana na amepania kuziadabisha.
“Mtibwa ipo vizuri kwa kuleta ushindani kwenye
ligi na kwa upande wangu, nimejipanga kurejesha makali yangu niliyokuwa nayo
kabla ya kwenda Yanga.
“Najua hizo timu kubwa zinatamba kila siku kuwa
na vikosi imara, lakini najua tutakachozifanya na hilo litakuwa fundisho kwao
kudharau wachezaji zilizokuwa nao,” alisema Bahanuzi.
Katika kikosi cha Mtibwa, Bahanuzi yupo na
Hussein Javu ambaye walikuwa wote Yanga lakini hawakuweza kupata nafasi katika
kikosi cha kwanza.







0 COMMENTS:
Post a Comment