Mwenyekiti
wa kamati ya Usajili ya Simba, Zacharia Hans Poppe ameibuka na kuamsha jambo
jipya sana, kwamba wapi ambako watani wao Yanga wanatoa mamilioni ya fedha na
kufanya usajili.
Hans
Poppe amesema Yanga imekuwa klabu inayopandisha kwa kasi kubwa fedha za
mishahara na zile za usajili wa wachezaji kutoka nje, jambo linalofanya
ajiulize, wanatoa wapi hizo fedha.
Katika
mahojiano maalum na SALEHJEMBE, Hans Poppe amesema Simba na Yanga ni klabu ambazo
vyanzo vyao vya mapato vinalingana kabisa.
“Lakini
wenzetu wamekuwa wakiwalipa wachezaji hasa wa nje zaidi ya mara mbili. Jambo
ambalo linaonyesha wazi kuna kitu, najiuliza wanatoa wapi fedha.
“Tambwe
ambaye amekuwa akilipwa dola 800 (Sh milioni 1.6), Yanga nasikia wanamlipa dola
2,000 ( Sh milioni). Najiuliza sana, kwamba tunapokwenda ni tatizo pia,”
alisema Hans Poppe.
“Angalia
wachezaji wa Burundi tulikuwa tukiwasajili kwa fedha ya chini, Yanga wameingia
na papara na kupandisha sana masuala ya usajili.
“Nakumbuka
hata Azim Dewji na Abbas Guramali walipandisha sana fedha za mishahara na
usajili. Baada ya wao kuondoka, waliobaki walisumbuka sana.
“Ningependa
kuwaasa viongozi wa Yanga kuliangalia hilo, au Yanga iwe makini kwamba kweli
fedha hizo zinazotoka ni zile zinazotokana na kipato chao.
“Hauwezi
ukawa mfanyabishara makini halafu ukawa unalipa zaidi ya kile unachoingiza nah
ii ndilo swali langu la msingi,” alisisitiza Hans Poppe.
“Najua
kwenye hizi klabu kuna watu wanasaidia, lakini najua si kwa namna hivyo.”
Hans
Poppe alisema msimu huu, usajili wa Simba umefanyika kwa kufuata utaratibu na
bajeti ambayo inaingia ndani ya kipato cha Simba.
“Kweli,
hatukutoka nje ya kipato chetu. Ni usajili ambao umefiti ndani ya kipato cha
Simba,” alisisitiza Hans Poppe.
Simba
inafungua dimba la Ligi Kuu Bara dhidi ya African Sports katika mechi
itakayochezwa kwenye Uwanja wa Mkwakwani mjini Tanga, leo.







0 COMMENTS:
Post a Comment