Siku
chache baada ya kuonekana katika mazoezi ya Azam FC, kipa mkongwe Ivo Mapunda,
juzi Jumatano alionekana katika mazoezi ya Toto Africans kwenye Uwanja wa Chuo
cha Ualimu Butimba akiwanoa makipa wa timu hiyo.
Kipa huyo
wa zamani wa Yanga na Simba, alionekana akiwa bize muda mwingi ambapo alisema
kuwa yupo Mwanza kwa mapumziko ya wiki moja.
“Nimekuja
kupumzika lakini kwa kuwa mimi ni mchezaji, nimeona siyo mbaya nikifanya
mazoezi na wenzangu, natagemea kuondoka Ijumaa (leo) kurejea Dar es Salaam
ambako nitafanya mazoezi na Azam FC,” alisema Ivo.
Awali, Ivo
alialikwa kwenda kufanya mazoezi katika kikosi cha AFC Leopards cha Kenya
kinachonolewa na kocha wa zamani wa Simba, Zdravko Loagarusic.







0 COMMENTS:
Post a Comment